Ghaibu iko kwa Mwenyezi Mungu hakuna aijuaye ila Yeye, na ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa funguo za mambo yaliyofichikana na hazina zake ni tano: Ya kwanza: Hakuna ajuaye ni lini kitasimama Kiyama isipokuwa Mwenyezi Mungu, ikiashiria kuijua Akhera, kwani siku ya Kiyama ndio mwanzo wake, na ikikanushwa elimu ya kilicho karibu basi inashindikana elimu iliyo baada yake. Ya pili: Hakuna ajuaye ni lini inakuja mvua isipokuwa Mwenyezi Mungu, hii ikiashiria mambo ya ulimwengu wa juu, na ameitaja mvua pekee pamoja nakuwa inaweza kuwa na sababu zilizozoeleka zinazoweza kujulisha unyeshaji wake lakini hua hazina uhakika wala yakini. Ya tatu: Yanayokuwa katika mifuko ya uzazi; kama mwanaume au mwanamke, mweusi au mweupe, amekamilika maumbile au amepungua, muovu au mwema na mfano wake, na ametaja uzazi pekee kwa sababu kwa kawaida watu wengi wanaujua, pamoja na hivyo akakanusha yeyote kujua uhalisia wake basi kisichokuwa mfuko kutojulikana ndio bora zaidi. Ya nne: Hakuna ajuaye yaliyoko kesho isipokuwa Mwenyezi Mungu, ikiashiria aina za nyakati na matukio yaliyomo, na ameeleza kwa tamko "kesho" ili uhalisia wake uwe ni wakati wa karibu zaidi, na ikiwa pamoja na ukaribu wake hakuna ajuaye uhalisia wa yatakayotokea ndani yake, pamoja na kuwezekana kupata dalili na alama zake, basi siku baada yake ndio bora zaidi kutojulikana. La tano: Haijui nafsi itafia nchi gani, ikiashiria mambo ya ulimwengu wa chini, pamoja nakuwa kawaida watu wengi hufia katika nchi zao, lakini hilo si uhalisia, bali lau atakufa katika nchi yake pia hajui ni Ardhi gani atazikwa, hata kukiwa na makaburi ya watangulizi wake, "Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mwenye habari" ameyazingira yenye kuonekana na yasiyoonekana, na yaliyofichikana na yaliyohifadhiwa, na siri zote, aya ikakusanya aina mbali mbali za ghaibu, na ikaondoa madai yote mabovu.